Hifadhi ya Bahari Ya ghuba ya Mnazi na Maingilio ya Mto Ruvuma imeshirikiana na wadau mbalimbali wa uhifadhi katika shughuli ya uoteshaji wa mikoko

Wiki hii Mnazi Bay kwa kushirikiana na wadau mbalimbali walishirikiana katika upandaji wa mikoko katika eneo la hekta tano za kijiji cha Msimbati, Viongozi wa halmashauri za vijiji na VLCs waliahidi kuchukua juhudi zao za dhati kuhakikisha mikoko iliyorejeshwa inakua vizuri na kulindwa.