MAFUNZO YA UKUSANYAJI WA TAKWIMU ZA SAMIKI KIDIGITALI
![MAFUNZO YA UKUSANYAJI WA TAKWIMU ZA SAMIKI KIDIGITALI](http://marineparks.eganet.go.tz/uploads/news/1bafe3c700e908f084bc183d23d5ca8d.jpeg)
Mafunzo ya ukusanyaji takwimu kwa njia ya kidigitali katika mfumo wa eCAS yakiedelea. Mafunzo haya ni ya muda wa siku 10 kuanzia tarehe 16/10/2023 hadi 26/10/2023, jumla ya washiriki 12 ambao ni wakusanya takwimu 6 kutoka katika vijiji vya Chemchem, Mibulani, Kiegeani, Bwejuu na Jibondo pia wafanyakazi 6 kutoka katika Hifadhi ya Bahari ya Mafia. Mafunzo haya yanatolewa na wakufunzi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Taasisi ya Utafiti (TAFIRI) pamoja na IT kutoka MPRU.